google.com, pub-4324601895065941, DIRECT, f08c47fec0942fa0

Habari Mpya

6/recent/ticker-posts

MAELFU YA WATU WAVUNJA NGUVU YA CHAKULA CHA KICHAWI KWENYE MAISHA YAO, NDANI YA BONDE LA KUKATA MANENO KAWE.




IBADA YA JUMAPILI TAREHE27/07/2014
MCHUNGAJI KIONGOZI JOSEPHAT GWAJIMA
SOMO: CHAKULA CHA KICHAWI
                                                            I.                    UTANGULIZI.
Mchungaji kiongozi  Josephat Gwajima
Danieli 1:1-21
Kweye biblia neno chakula limeandikwa mara 185  na neno usile limeandikwa mara 15 na shetani hana nguvu juu  ya watu wa Mungu mpaka anapopata nafasi na shetani amepata nafasi kubwa sana kwenye chakula kwa kuwaangamiza watu na kuna aina mbili za chakula chakula cha kiroho na chakula cha kimwili  1wakorintho10: 1 Kwa maana, ndugu zangu, sipendi mkose kufahamu ya kuwa baba zetu walikuwa wote chini ya wingu; wote wakapita kati ya bahari; 2 wote wakabatizwa wawe wa Musa katika wingu na katika bahari; 3 wote wakala chakula kile kile cha roho; 4 wote wakanywa kinywaji kile kile cha roho; kwa maana waliunywea mwamba wa roho uliowafuata; na mwamba ule ulikuwa ni Kristo. 5 Lakini wengi sana katika wao, Mungu hakupendezwa nao; maana waliangamizwa jangwani. 6 Basi mambo hayo yalikuwa mifano kwetu, kusudi sisi tusiwe watu wa kutamani mabaya, kama wale nao walivyotamani. 7 Wala msiwe waabudu sanamu, kama wengine wao walivyokuwa; kama ilivyoandikwa, Watu waliketi kula na kunywa, kisha wakasimama wacheze. 8 Wala msifanye uasherati, kama wengine wao walivyofanya, wakaanguka siku moja watu ishirini na tatu elfu. 9 Wala tusimjaribu Bwana, kama wengine wao walivyomjaribu, wakaharibiwa na nyoka. 10 Wala msinung'unike, kama wengine wao walivyonung'unika, wakaharibiwa na mharabu. 11 Basi mambo hayo yaliwapata wao kwa jinsi ya mifano, yakaandikwa ili kutuonya sisi, tuliofikiliwa na miisho ya zamani. 12 Kwa hiyo anayejidhania kuwa amesimama na aangalie asianguke. 13 Jaribu halikuwapata ninyi, isipokuwa lililo kawaida ya wanadamu; ila Mungu ni mwaminifu; ambaye hatawaacha mjaribiwe kupita mwezavyo; lakini pamoja na lile jaribu atafanya na mlango wa kutokea, ili mweze kustahimili. 14 Kwa ajili ya hayo, wapenzi wangu, ikimbieni ibada ya sanamu. 15 Nasema kama na watu wenye akili; lifikirini ninyi ninenalo. 16 Kikombe kile cha baraka tukibarikicho, je! Si ushirika wa damu ya Kristo? Mkate ule tuumegao, si ushirika wa mwili wa Kristo? 17 Kwa kuwa mkate ni mmoja, sisi tulio wengi tu mwili mmoja; kwa maana sisi sote twapokea sehemu ya ule mkate mmoja. 18 Waangalieni hao Waisraeli walivyokuwa kwa jinsi ya mwili; wale wazilao dhabihu, je! Hawana shirika na madhabahu? 19 Basi niseme nini? Ya kwamba kile kilichotolewa sadaka kwa sanamu ni kitu? Au ya kwamba sanamu ni kitu? 20 Sivyo, lakini vitu vile wavitoavyo sadaka wavitoa kwa mashetani, wala si kwa Mungu; nami sipendi ninyi kushirikiana na mashetani. Hamwezi kunywea kikombe cha Bwana na kikombe cha mashetani. 21 Hamwezi kushirikiana katika meza ya Bwana na katika meza ya mashetani. Biblia ukisema chakula cha kiroho unaweza kutafasiri mambo mawili yani chakula cha rohoni yani chakula cha kiroho. Lakini ni chakula gani kimeitwa chakula cha kiroho kulikuwa na vipande vya mikate vidogovidogo walikula chakula hichohicho tangu waanze safari mpaka mwisho wa safari kwamaana kwamba kulikuwa na nguvu kwenye chakula hicho kunakuwa na nguvu ndani ya chakula hichi kinaonekana cha kimwili ni cha kawaida lakini ndaniyake kuna nguvu za Mungu na anayekula anaonekana ana kula chakula chenye virutubisho.

Hata ukiwa Japani ufufuo na uzima pia inapatikana.
II.                  SOMO.
Ndani ya chakula kunaweza kuwa na mauti na uzima. Baada ya Israeli kuvamiwa wana wa Israeli walipelekwa mpaka nchi ya Babeli (Iraq) utumwani. Walipofika babeli walilazimishwa kula chakula ambacho kimetolewa sadaka kwa  miungu na akinadanieli wakaambiwa wabadilishe majina yao na kabla mfalme hajala kile chakula cha mfalme kinachukuliwa alafu kinaombewa kitu Fulani kwamba mtu atakapokula awe mtu wa aina Fulani, Yesu alisema yeye alayee chakula changu anauzima alafu akasema Baba zenu walikula chakula wakafa lakini mimi ninachakula cha uzima sasa wewe unapokaribishwa kwenye chakula ambacho kimenuiziwa mambo ya kichawi mambo ya kishetani unapatwa na kansa, magonjwa na matatizo na leo ni mwisho.
Yohana6: 46 Wale watumishi wakajibu. Hajanena kamwe mtu ye yote kama huyu anavyonena. 47 Basi Mafarisayo wakawajibu, Je! Ninyi nanyi mmedanganyika? 48 Ni nani katika wakuu amwaminiye, au katika Mafarisayo? 49 Lakini makutano hawa wasioifahamu torati wamelaaniwa. 50 Akawaambia Nikodemo, (naye ni yule aliyemwendea zamani, maana ni mmoja wao), 51 Je! Torati yetu humhukumu mtu kabla ya kumsikia kwanza, na kujua atendavyo? 52 Wakajibu, wakamwambia, Je! Wewe nawe umetoka Galilaya! Tafuta, ukaone ya kuwa kutoka Galilaya hakutokea nabii.
Hata alipokuwa na wanafunzi wake aliwaonyesha kwa kuchukua mkate na kuwaambia yeye aulaye mwili wangu atakuwa na uzima wa milele na kwasababu hiyo ule mkate uliingia nguvu ya Yesu kristo unaingia ndani yake. Shetani ni malaika wa ngazi ya kerubi.
Yuda1: 6 Na malaika wasioilinda enzi yao wenyewe, lakini wakayaacha makao yao yaliyowahusu, amewaweka katika vifungo vya milele chini ya giza kwa hukumu ya siku ile kuu., Ufunuo12: 7 Kulikuwa na vita mbinguni; Mikaeli na malaika zake wakapigana na yule joka, yule joka naye akapigana nao pamoja na malaika zake;   malaika wanasifa mojawapo ya kugeuza maumbo. Ndiomaana Ibrahumu aliwapokea malaika wenye maumbo ya watu na mavumbi na akawaandalia chakula wale mabwana wakakaa na kusubiria chakula wakala, sio kila mwenye mavumbi miguuni ni mtu, sio kila anayepiga stori ni mtu, ndiomaana kwenye chakula unaweza kula chakula kilicho nuiziwa unakula balaa, magonjwa, ajali, mauti, bila ya kujua.

Hesabu25: 2 kwa kuwa waliwaalika hao watu waende sadakani, sadaka walizowachinjia miungu yao; watu wakala chakula, wakaisujudu hiyo miungu yao. 3 Ikawa Israeli kujiungamanisha na Baal-peori; hasira za Bwana zikawaka juu ya Israeli. 4 Kisha Bwana akamwambia Musa, Watwae wakuu wote wa hao watu, ukamtungikie Bwana watu hao mbele ya jua, ili kwamba hizo hasira kali za Bwana ziwaondokee Israeli. 5 Basi Musa akawaambia waamuzi wa Israeli, Waueni kila mtu watu wake waliojiungamanisha na Baal-peori.
Chakula mtu anakitoa sadaka kwa mashetani kinanuiziwa mfano kwenye mila wanachukua pombe na mtama wanakunywa wanaongea maneno maanayake wanatoa sadaka na mashetani, majini, mapepo ugali, pilao, au chakula chochote na unapokula wanaingia mwilini na kufanya kazi ya uharibifu na wewe na hayo mashetani mnakuwa kitu kimoja.
Kuna watu wengi wagonjwa kwasababu ya chakula na Matendo ya mitume15:20 bali tuwaandikie kwamba wajiepushe na unajisi wa sanamu, na uasherati, na nyama zilizosongolewa, na damu.
1Wakorintho10: 20 Sivyo, lakini vitu vile wavitoavyo sadaka wavitoa kwa mashetani, wala si kwa Mungu; nami sipendi ninyi kushirikiana na mashetani. Hamwezi kunywea kikombe cha Bwana na kikombe cha mashetani. 21 Hamwezi kushirikiana katika meza ya Bwana na katika meza ya mashetani. 22 Au twamtia Bwana wivu? Je! Tuna nguvu zaidi ya yeye? 23 Vitu vyote ni halali; bali si vitu vyote vifaavyo. Vitu vyote ni halali; bali si vitu vyote vijengavyo.
1Wafalme19:1 Basi, Ahabu akamwambia Yezebeli habari ya mambo yote aliyoyafanya Eliya, na jinsi alivyowaua manabii wote kwa upanga. 2 Ndipo Yezebeli akampelekea Eliya mjumbe, kusema, Miungu wanifanyie hivyo na kuzidi, nisipokufanya roho yako kesho, panapo wakati huu, kama roho ya mmojawapo wa hao. 3 Naye alipoona hayo, aliondoka, akaenda aihifadhi roho yake, akafika Beer-sheba, mji wa Yuda, akamwacha mtumishi wake huko. 4 Lakini yeye mwenyewe akaendelea katika jangwa mwendo wa siku moja, akaenda akaketi chini ya mretemu. Akajiombea roho yake afe, akasema, Yatosha; sasa, Ee Bwana, uiondoe roho yangu; kwa kuwa mimi si mwema kuliko baba zangu. 5 Naye akajinyosha akalala chini ya mretemu; na tazama, malaika akamgusa, akamwambia, Inuka, ule. 6 Akatazama, kumbe! Pana mkate umeokwa juu ya makaa, na gudulia la maji, kichwani pake. Akala, akanywa, akajinyosha tena. 7 Malaika wa Bwana akamwendea mara ya pili, akamgusa, akasema, Inuka, ule; maana safari hii ni kubwa mno kwako. 8 Akainuka, akala, akanywa, akaenda katika nguvu za chakula hicho siku arobaini mchana na usiku hata akafika Horebu, mlima wa Mungu.
Kumbe unaweza ukapewa chakula cha kishetani ukatembea kwenye balaa kwa chakula hicho mpaka ukaingia mautini na unatakiwa uangalie pale unapokaribishwa chakula kunauzima humo. Lazima ujue mitego ya mwindaji kwingine umefanikiwa lakini anaweza kukukamata kwenye chakula na unatakiwa useme “Baba Mungu ninaweka Baraka kwenye chakula hiki kwa jina la Yesu”.
Kunaweza kuwa na mauti na mauti sio tukio mauti ni roho ni jini kumbuka wana wa manabii waliona roho ya mauti kwenye sufuria.  Mtu anaweza akanuizia jambo Fulani kwenye chakula. Kama Mungu alivyo na watu wake na shetani naye ana watumishi wake. Wakiona imeshindikana kukuletea chakula wanaanza kukuletea ndotoni, ndiomaana unakuta mtu anatafuna akiwa amelala. Tulipookolewa tunalindwa na Mungu kwa njia ya Imani na ndio maana unapotaka kulala lazima uombe na sio useme Bwana Yesu shuka utulinde hapa! Tunaotenda kazi ni sisi tena kwa ujasiri unawaamuru malaika wakulinde.
“Kwa jina la Yesu ikiwa tatizo langu lilianza kwenye chakula nilichopewa kuanzia leo ninakataa kwa jina la Yesu” ndoto ni bayana hakuna aliyeota hakikutokea kina Ebimeleki,yusufu utawala, farao njaa, nebkandneza, askari wa jeshi la midiani kwa mikate iliyoanguka toka mbinguni, hakuna aliyeota ndoto haikutokea. Kama uko imara ndotoni unaota umekaribishwa lakini wewe huli maana yakee uko imara. Wanaolishwa chakula ndotoni kama uko juu unashushwa chini, kama unakazi unaipoteza kazi hiyo, kushindwa kuomba.
Kunawatu wengi wamelishwa chakula nyumbani kwa mtu na wameharibikiwa maisha yao ”kwa jina la Yesu  kuanzia leo magonjwa niliyoyapata kwa kulishwa chakula ndoton ninayakataa kwa jina la Yesu mahala popote nilipokula chakula cha kichawi kuanzia leo enyi mashetani mlioniwekea kutokuolewa kutokufanikiwa kuanzia leo ninawafyeka kwa jina la Yesu navunja maagano yaliyokuwa ndani ya chakula ninayavunja kwa jina la Yesu maagano ya mauti, maagano ya kifo ninayavunja kwa jina Yesu ninaagiza kuanzia sasa majini, majoka , mizimu walionuiziwa kwenyee chakula cha ndotoni, kwenye chakula cha mwilini kuazia leo ninakataaa kwa jina la Yesu”.( ukitaka kutatua tatizo unatakiwa ujue chanzo cha tatizo”)
Wengine  kwa njia ya chakula wanaweza kuchukua nyota yako wananuizia kabisa na hakuna kinachotokea chenyewe vitu vinatengenezwa ndio maana duniani
                                Kuna watu wa aina tatu.
1.       Wale wanaoona matukio yanatokea tu lakini hawajuwi kinachoendelea.
2.       Wale wanaojua kinachoendelea; wakiona nchi wanajua kinachoendelea wakiona mtu kafa wanajua kinachoendelea
3.       Watu wanaotengeneza mambo yatokee wakitaka upatwe ugonjwa unapatwa na ugonjwa.
Tukidili na chanzo cha tatizo tunalimaliza tatizo, kuna mamlaka ya rohoni inayotegemewa kusimamisha mambo Fulani. Maisha ya mtu hujulikana kabla hayajaanza; Yeremia anasema  Kabla sijakuumba katika tumbo nalikujua, na kabla hujatoka tumboni, nalikutakasa; nimekuweka kuwa nabii wa mataifa. Inawezekana wamekupotezea miaka mingi lakini Mungu anaweza kukurudishia vyote vilivyopotea, Mungu ni Mungu wa nafasi ya pili na usiangalie vile ulivyo Biblia inasema amelaaniwa yeye amtegemeaye mwanadamu kwa jambo lolote.
Baraka ndani ya chakula na laana ndani ya chakula, kabla hujazaliwa Baraka zako zinaonekana ukiwa tumboni mwa mama yako. Kuna wakati mwingine mtu huwa hapendi lakini hubalansi kwasababu ya urafiki, kuna mambo unakula leo halafu madhara yanaanza mwaka kesho. Haung’ai kwasababu unavyoonekana kwa nje hapana bali kuna kitu kimewekwa ndani yako na Mungu na wachawi hukiona na kukichukua na wewe unadhani unafanyiwa fitina kumbe ulipewa chakula kilichonuiziwa.
Kilichowekwa ndani yako kinakupigisha hatua kwa elimu na kisipokuwepo unakuta unasoma lakini hauwezi kufanikiwa kumbe ni chakula. “Kwa jina la Yesu ninajikinga na chakula au vinywaji au kitu chochotee kilichotolewa sadaka kwa mashetani na mtu yeyote aliyetoa sadaka ninamteketeza kwa jina la Yesu chochote alichonipa mtu ndugu rafiki au mtu yeyote bila kujua nikala au nikanywa kuanzia leo yamrudie yeye mwenyewe kwa jina la Yesu” unamatatizo na haujui matatizo hayo yanatokea wapi na kuwa wa kwanza darasani sio kuwa na maisha mazuri lakini Mungu ameweka kitu ndani ya mtu nyota uwezo karama imewekwa ndani ya mtu na elimu inamsaidia mtu huyo. Kila chakula unachokula lazima kiwe kimetolewa sadaka mahali Fulani na ndio maana watu wa Mungu wanapotaka kula wanakiombea “kwa jina la Yesu  ninawashinda wote walioandaa chakula wiki hii kwenye ndoto, kwenye sherehe nawashinda kwa jina la Yesu”
Unapokaribishwa chakula lazima uangalie unaweza kula kilichonuiziwa na shida watu wamezoea kuombewa, unatakiwa ujifunze kupigana wewe mwenyewe unapiganaje unapigana kwa jina la Yesu”kwa jina la Yesu kila chakula kilichoandaliwa kichukue nyota naamuru roho yangu ikatae kwa jina la Yesu. Kwa jina la Yesu kila aliyeandaa chakula cha mauti, kinywaji cha kifo namrudishia yeyee kwa jina la Yesu  aliye andaa kwenye ndoto au mahala popote ninakataa kwa jina la Yesu” kila unachosema kinakuwa.
Kwanini ninasisitiza kuomba mathayo10: 8 Pozeni wagonjwa, fufueni wafu, takaseni wenye ukoma, toeni pepo; mmepata bure, toeni bure. Kila mtu aliyempokea Yesu anauwezo 1 Akawaita wanafunzi wake kumi na wawili, akawapa amri juu ya pepo wachafu, wawatoe, na kupoza magonjwa yote na udhaifu wa kila aina. Marko7:6 luka 10:19  Tazama, nimewapa amri ya kukanyaga nyoka na nge, na nguvu zote za yule adui, wala hakuna kitu kitakachowadhuru. Kwahiyo usiseme niombeeni unatakiwa uvunje mwenyewe kama unamjua mchawi unamtaja na jina Mathayo18: 18 Amin, nawaambieni, yo yote mtakayoyafunga duniani yatakuwa yamefungwa mbinguni; na yo yote mtakayoyafungua duniani yatakuwa yamefunguliwa mbinguni. Vita vya rohoni ni kwamba wewe unaomba ukitaja maneno na utakuwa vile unavyoamini. Sisi mbele za Mungu ni watoto wa Mungu na Mungu hutenda sawa na vile vile unavyoamini, ukiamini nikimfunga shetani anafungika na inakuwa hivyo hivyo ulivyoamini.
III.                UKIRI
Baba wa mbinguni nimeisikia sauti yako na ninaomba nguvu ya uweza kushindana na wakala wote wa shetani na kila mtu aliye nihusisha  kwa jambo lolote la kuweza kunisababishia uharibifu ndani yangu  leo ninaomba asipate nguvu juu yangu na kwasababu hiyo ninapokea nguvu  na kujitakasa.
Maelfu ndani ya bonde la kukata maneno kawe


IV.                MAOMBI
Katika jina la Yesu kristo mwana wa Mungu aliye hai ninavunja mashetani yote yaliyoingizwa kwenye familia  yangu kwa njia ya  chakula kwa jina la Yesu. Ninasambaratisha kuanzia sasa magonjwa yaliyopandwa kwa njia ya chakula ninayaharibu na kuyaangamiza kwa jina la Yesu, kila kufeli, kuanguka kulikosababishwa kwa njia ya chakula ninasimama kinyume nacho kwa damu ya mwana Kondoo, kila kinywaji nilichokinywa   kila kushindwa kulikosababishwa kwasababu ya  chakula ninasambaratisha kwa jina Yesu, ninaharibu wasimamizi wa chakula mlioungamanishwa na chakula kwa damu ya mwanakondoo, ninafungua vingufungo vyote vilivyofungwa na wakala wa shetani kwenyee familia yangu na maisha yangu kwa njia ya chakula ninabomoa kwa damu ya mwanakondo katika jina la Yesu, mauti iliyoingia kwa njia ya chakula ninaiharibu kwa jinala laYesu, ninaharibu udhaifu wowote ulionuiziwa kwenye chakula juu yangu kwa damu ya mwana kondoo, “vita sio vyangu vita ni vya Bwana” ninaharibu kila chanzo cha magonjwa, mikosi, kukataliwa, ninafungua kamba zote katika jina la Yesu. Kwa jina la Yesu kila atakaye niletea zawadi au chakula kwa njia ya siri naiamuru laana ile imrudie yeye kwa jina la Yesu lakini mimi sitalogwa kwa jina la Yesu.
                  AMEN.

Post a Comment

2 Comments

  1. bwana apewe sifa ,salom ,asante mtumishi wa mungu kwa somo la leo lime nigusa sana

    ReplyDelete
  2. Ubarikiwe sana dady tunakupenda sanaaaaa... from media crew Dodoma.

    ReplyDelete