Na: Pastor Josephat Gwajima
1 Wakorintho 1:18- Kwasababu neno la msalaba kwao wanaopotea
ni upuuzi bali kwetu sisi tunaookolewa ni nguvu ya Mungu.
“UJUMBE WA MSALABA NI NGUVU YA MUNGU” nilikua najiuliza sana
neno la msalaba maana yake nini, nikajiuliza hivi ni kwanini Yesu alisulubiwa
msalabani, kwanini asingepigwa mawe au makonde mpaka akafa.?
Tunaanza kuona msalaba ni wa muhimu sanandio sababu biblia inasema katika
Yohana 19:17 “Akatoka
hali akijichukulia msalaba wake mpaka mahali palipoitwa fuvu la kichwa au kwa
Kiebrania goligotha”
Yesu alipoonekana anatakiwa kusulubiwa alitolewa nje ya mji
akasulubiwa kwenye mlima mmoja mahali palipoitwa kalvari ambapo palikua ni
mlimani, na si Yesu peke yake aliyesulubiwa mahali hapo bali walikuwepo
wanyanganyi wawili, aliyekua mtakatifu akasulubiwa pamoja na wanyang'anyi
Mahali hapo palikua si bondeni bali ni katika mlima na
ilikua karibu na njia, na wakati huo wayahudi walikua wakisherekea sikukuu ya
pasaka, yeye naye akasulubiwa katika sikukuu hiyo ya pasaka.
Wayahudi waliokua wanaingia mjini wote kwasababu ya sikukuu
walimuona njiani hapo akiwa ametundikwa uchi mbele za watu wote kwasababu mahali hapo palikua ni njiani.
Mtu ambaye alikua anafufua, mtu ambaye alikua anaponya, mtu
ambae alikua analisha watu maelfu leo amevuliwa nguo na ametundikwa katika mti kwa misumali.
Waliona mtu huyu ametusumbua sana tukimuua hivi hivi aibu
yake haitaonekana vizuri ni bora tumuinue katika mti ili aonekane na watu wote,
watu wengine waliokua wakipita njiani kila walipomuona walikua wakitema mate
chini, na wengine wakisema aliokoa wengine basi na ajiokoe mwenyewe.
Na zaidi ya hapo wakamvisha taji ya miiba na kumchapa sana,
mgongoni alipigwa viboko thelathini na tisa, ukimuangalia amejaa damu na yuko
uchi.
Wanafunzi wake wakimuangalia aliyekua kiongozi wao mbele ya
askali waliokuia wakimdhihaki mbele ya watu wote, na watu wakasema amekomeshwa,
wakasema amewezwa na kila mtu akasema aliyoweza kwasababu ulikua ni wakati wa aibu.
Kwenye maisha Mungu anaweza akaruhusu wakati wa aibu,
ukaaibika na ukakosa msaada, wale wanafunzi waliotembea na Yesu walimuona
akiaibika lakini walikua hawana msaada, Lazaro aliyefufuliwa alikuwepo lakini
alikua hana msaada, wanaume elfu tano aliowalisha hawakuweza kutoa msaada, wale
wakoma kumi aliowatakasa walikuwepo lakini walikua hawawezi kutoa msaada.
Na wote waliokua wakimtakia mabaya wakafurahi wakaona tumemkomesha na tumemuweza. Na Mungu
wa mbinguni alipoona mwanae ameaibika amebeba dhambi za ulimwengu akamgeuzia mgongo,
yeye ambae alimtegemea amsaidie naye akamgeuzia mgongo, akabaki peke yake, ndio sababu akalia akasema BABA YANGU BABA
YANGU MBONA UMENIACHA
Wakasema alisema yeye ni mwana wa Mungu lakini hata baba
yake amemuacha, na amesema mwenyewe. Bwana Yesu alikufa huku analalamika kwenye aibu
mlimani.
Na alipokua katika hiyo aibu Mungu wa mbinguni hakuweza
kuvumilia akaweka akaamua kulifunika jua na giza likaingia duniani ili kuificha
aibu.
Baada ya kuona ameitimiza aibu yote akapaza sauti akasema
imekwisha na akakata roho.
Yawezekana umepata jambo likakuletea aibu ya asilimia mia
moja na wale wote niliokua nikiwategemea wameniacha, wewe sio wa kwanza hata
Yesu alipitia katika hali hiyo.
Baada ya hapo Yesu akazikwa, na katika msiba wake hakuzikwa
na watu wengi alizikwa na mtu mmoja aliyekua anaitwa Yusufu, mtu ambae alienda kuuomba mwili kwa pilato ili akauhifadhi.
Baadae wakaamuru kabuli lake lilindwe, hata baada ya kufa
wakataka kuendelea kuilinda aibu yake.
Kumbe unaanza kujifunza kuna aibu unaweza ukawa umeipata
katika maisha yako, aibu ya ndoa, au ya masomo au aibu ya aina yoyote wako
walinzi wa rohoni ambao kazi yao ni kuendelea kukulinda katika aibu hiyo hiyo
ili uendelee kuabika.
Napenda kukupa habari njema ULIABIKA MLIMANI, UTATUKUZWA
MLIMANI PIA.
Wapo watu wanaoendelea kuilinda aibu yako ili iendelee vile
vile, ila leo napenda kukuambia uliaibika mbele ya watu wote na utukufu wako
utaonekana mbele ya watu wote pia .
Yawezekana ulichumbia na mahali ikatolewa lakini kabla ya
ndoa uchumba ukavunjika, au ulikua mfanya biashara mzuri lakini baada ya muda
ukapoteza kila kitu na unaona aibu kuwaambia watu kuwa biashara imekufa, pale
pale ambapo shetani anakazania uaibikie hapo Mungu naye anataka usiabike kwa
jina la Yesu.
Baada ya siku tatu tukio moja likatokea wakati walinzi
wanailinda ile aibu, panapo majira ya asubuhi wakaanza kuhisi tetemeko la nchi
wakamuona malaika akishuka mwenye sura kama umeme akashuka na wale walinda aibu
wakaanza kutetemeka na kuwa kama wamekufa.
Leo ni maombi yangu kila wanaoilinda aibu yako waanze
kutetemeshwa na wawe kama wamekufa kwa jina la Yesu.
NINAIONA AIBU YAKO INAANZA KUONDOKA KWA JINA LA YESU
WALE WANAOILINDA AIBU YAKO WAOGOPE WATETEMKE NA WAWE KAMA
WAFU KWA JINA LA YESU
Baada ya malaika kushuka Yesu akatoka kaburini na baada ya
kutoka kaburini yule malaika akalikalia lile jiwe, hii ni kwasababu baada ya
aibu kuna uthibitisho baada ya unaokuwepo.
Baada ya Yesu kufufuka alikaa na wanafunzi wake siku arobaini
na akawachukua wanafunzi wake akaenda nao katika mlima wa mizeituni akapanda
nao mlimani akiwa na mwili wa utukufu, akiwa amejaa utukufu mwingi akapaa
kwenda mbinguni.
Aliabika mlimani na alitukuzwa mlimani, mahali pale ambapo
kila mtu alimuona wakati anaaibu wakamuona akiwa katika utukufu mbele ya watu
wote.
Yawezekana tatizo lako limejulikana na watu wote wakati
unaaibika lakini kama yesu alivyoaibika nba kutukuzwa mlimani n akwako pia
utatukuzwa mbele ya watu wote.
UKIAIBIKA WAZI WAZI UTATUKUZWA WAZI WAZI.
Yesu aliwaambia watu ni mwana wa Mungu wakampiga na kumuua
mbele ya watu wote, Mungu akadhihirisha mbele ya watu wote kwa kulituma wingu
kutoka kwake lije kumchukua mbele ya watu wote.
Yawezekana umeaibishwa sana na kufedheheshwa sana lakini
mungu nae anaompango wa kukutukuza mlimani mbele ya watu wote
Aibu uliyoipata itaondoka kwako na furaha yako itarejea tena
kwa jina la Yesu.
Musa alishindwa kuingia katika nchi ya ahadi na watu wakawa
wanajua Musa ameaibika kwa kushindwa kuirithi nchi ya ahadi lakini wakati Yesu
yuko duniani katika nchi ile ile ya kanani Yesu alitokewa na Musa na Eliya
wakiwa katika utukufu mwingi.
Kuna wakati Mungu anaruhusu unapitia katika mambo makubwa
magumu ambayo yaaonyesha ni fedheha ya nmana ya ajabu lakini napenda ufahamu kadiri tatizo lako
linavyozidi kuwa kubwa ufumbuzi wako nao unakua mkubwa na wenye utukufu mwingi.
Ndio sababu ujumbe wa msalaba kwao wanaopotea ni upuuzi bali
sisi tunaookolewa ni nguvu ya Mungu, neon la msalaba hilo ni ile aibu ya
msalabani, mateso ya msalabani fedheha ya msalabani na Mungu alipoona ameaibika vya kutosha
akamtukuza kwa kumtumia wingu mbele ya watu wote na utukufu wake ukawa mkuu.
Ninaomba leo kila wanaokulinda kwenye aibu yako waaibike na
wawe kama wafu , na wewe utukuzwe juu sana kwa JIna la Yesu
0 Comments